Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa walioshikiliwa mateka waachiwa.

In Kimataifa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imearifu kuwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliokuwa wakishikiliwa mateka na wakimbizi kutoka Sudan Kusini, wameachiwa huru wakiwa salama.
Wafanyakazi hao 16 walikuwa wakishikiliwa na kundi la waasi wa zamani kutoka Sudan Kusini, waliokuwa wafuasi wa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Riek Machar, na ambao waliikimbia nchi yao baada ya kuzuka mapigano baina yao ya wanajeshi wa serikali ya Rais Salva Kiir.
Wakimbizi hao walikuwa wakishinikiza kupelekwa katika nchi nyingine, kuepuka msongamano katika kambi ndogo wanakohifadhiwa Mashariki mwa Kongo.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa Wasudan Kusini wapatao milioni tatu wameyapa kisogo maskani yao, wakikimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoripuka mwaka 2013, baada ya Rais Kiir kumfukuza makamu wake, Riek Machar.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu