Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa walioshikiliwa mateka waachiwa.

In Kimataifa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imearifu kuwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliokuwa wakishikiliwa mateka na wakimbizi kutoka Sudan Kusini, wameachiwa huru wakiwa salama.
Wafanyakazi hao 16 walikuwa wakishikiliwa na kundi la waasi wa zamani kutoka Sudan Kusini, waliokuwa wafuasi wa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Riek Machar, na ambao waliikimbia nchi yao baada ya kuzuka mapigano baina yao ya wanajeshi wa serikali ya Rais Salva Kiir.
Wakimbizi hao walikuwa wakishinikiza kupelekwa katika nchi nyingine, kuepuka msongamano katika kambi ndogo wanakohifadhiwa Mashariki mwa Kongo.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa Wasudan Kusini wapatao milioni tatu wameyapa kisogo maskani yao, wakikimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoripuka mwaka 2013, baada ya Rais Kiir kumfukuza makamu wake, Riek Machar.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu