Ajali ya Lori yaua 7 Kigoma.

In Kitaifa
Watu saba wamefariki dunia katika ajali ya gari aina ya Scania iliyotokea katika Kijiji cha Mkongoro, Barabara ya Manyovu Wilaya ya Kigoma Vijijini.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva kushindwa kuimudu gari kwenye mteremko.
Amesema ajali hiyo imetokea jana Jumatano Machi 21, saa tatu asubuhi katika Mlima wa Kasagamba ambapo lori lenye namba T741AAB  lilianguka na kusababisha vifo vya watu saba akiwamo dereva wa gari hiyo aliyefahamika kwa jina la Siri Hamis (43) mkazi wa Singida pamoja na utingo wake aliyefahamika kama Ramadhani Saidi (23).
“Katika gari hiyo walikuwa wamebeba mizigo na watu wanne mmoja mwanamke na watatu wanamume ambapo wengine waliofariki na majina yao hayakufahamika mara moja.
“Ajali hiyo pia imesababisha kifo cha mwanafunzi aliyefahamika kwa jina la Eliakimu Samsoni (15 ), aliyekuwa akitembea kwa miguu kuelekea shuleni na gari hilo kumgonga akiwa anatembea,” amesema Kamanda Otieno.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu