Serikali ya Syria yakanusha vikali madai kuwa iliwachoma maelfu ya wafungwa kwa tanuri.

In Kimataifa

Duru mpya ya mazungumzo ya kutafuta amani Syria ilianza jana mjini Geneva huku serikali ya Syria ikanusha vikali madai kuwa iliwachoma maelfu ya wafungwa kwa tanuri katika gereza moja ili kuficha ushahidi wa mauaji ya maelfu ya wafungwa.

Duru tano zilizopita za mazungumzo ya kujaribu kuvimaliza vita vya Syria ambavyo vimedumu kwa zaidi ya miaka sita hazijaweza kufanikiwa kuutatua mzozo huo.

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Steffan Di Mistura alikutana jana na ujumbe wa serikali ya Syria na wa upinzani katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa.

Matumaini ya kuumaliza mzozo wa Syria ni madogo huku madai hayo kuwa maelfu ya wafungwa wanauawa na kisha kuchomwa katika gereza la Saydnaya yakizidisha uhasama kati ya pande mbili zinazozana.

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kukamilika mwishoni mwa wiki hii.

Vita vya Syria vimesababisha vifo vya zaidi ya watu laki tatu

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu