Maelfu ya watu wanaotoroka mapigano makali yanayoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wanamiminika katika nchi jirani ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya ghasia zinazochewa na uhasama wa kidini kuzuka katika mji wa mpakani wa Bangassou.

In Kimataifa

Maelfu ya watu wanaotoroka mapigano makali yanayoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wanamiminika katika nchi jirani ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya ghasia zinazochewa na uhasama wa kidini kuzuka katika mji wa mpakani wa Bangassou.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwashughulikia wakimbizi UNHCR limesema mmiminiko huo wakimbizi ni mkubwa na takriban watu 2,750 waliwasili kaskazini mwa Congo mwishoni mwa wiki iliyopita na wengine wengi bado wanawasili.

Wanajeshi sita wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa waliuawa katika mji huo wa Bangassou katika shambulizi lililofanywa na waasi wa kundi la Anti Balaka. Zaidi ya raia 100 pia waliuawa katika ghasia hizo kati ya makundi ya waasi ya Kikiristo na Kiislamu.

UNHCR imesema Congo ambayo yenyewe inakumbwa na ghasia tangu mwishoni mwa mwezi Machi, inawahifadhi wakimbizi zaidi ya laki moja kutoka Jamhuri ya Afrika ya kati.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu