Maelfu ya watu wanaotoroka mapigano makali yanayoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wanamiminika katika nchi jirani ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya ghasia zinazochewa na uhasama wa kidini kuzuka katika mji wa mpakani wa Bangassou.

In Kimataifa

Maelfu ya watu wanaotoroka mapigano makali yanayoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wanamiminika katika nchi jirani ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya ghasia zinazochewa na uhasama wa kidini kuzuka katika mji wa mpakani wa Bangassou.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwashughulikia wakimbizi UNHCR limesema mmiminiko huo wakimbizi ni mkubwa na takriban watu 2,750 waliwasili kaskazini mwa Congo mwishoni mwa wiki iliyopita na wengine wengi bado wanawasili.

Wanajeshi sita wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa waliuawa katika mji huo wa Bangassou katika shambulizi lililofanywa na waasi wa kundi la Anti Balaka. Zaidi ya raia 100 pia waliuawa katika ghasia hizo kati ya makundi ya waasi ya Kikiristo na Kiislamu.

UNHCR imesema Congo ambayo yenyewe inakumbwa na ghasia tangu mwishoni mwa mwezi Machi, inawahifadhi wakimbizi zaidi ya laki moja kutoka Jamhuri ya Afrika ya kati.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu