Serikali ya Syria yakanusha vikali madai kuwa iliwachoma maelfu ya wafungwa kwa tanuri.

In Kimataifa

Duru mpya ya mazungumzo ya kutafuta amani Syria ilianza jana mjini Geneva huku serikali ya Syria ikanusha vikali madai kuwa iliwachoma maelfu ya wafungwa kwa tanuri katika gereza moja ili kuficha ushahidi wa mauaji ya maelfu ya wafungwa.

Duru tano zilizopita za mazungumzo ya kujaribu kuvimaliza vita vya Syria ambavyo vimedumu kwa zaidi ya miaka sita hazijaweza kufanikiwa kuutatua mzozo huo.

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Steffan Di Mistura alikutana jana na ujumbe wa serikali ya Syria na wa upinzani katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa.

Matumaini ya kuumaliza mzozo wa Syria ni madogo huku madai hayo kuwa maelfu ya wafungwa wanauawa na kisha kuchomwa katika gereza la Saydnaya yakizidisha uhasama kati ya pande mbili zinazozana.

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kukamilika mwishoni mwa wiki hii.

Vita vya Syria vimesababisha vifo vya zaidi ya watu laki tatu

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu