Serikali ya Syria yakanusha vikali madai kuwa iliwachoma maelfu ya wafungwa kwa tanuri.

In Kimataifa

Duru mpya ya mazungumzo ya kutafuta amani Syria ilianza jana mjini Geneva huku serikali ya Syria ikanusha vikali madai kuwa iliwachoma maelfu ya wafungwa kwa tanuri katika gereza moja ili kuficha ushahidi wa mauaji ya maelfu ya wafungwa.

Duru tano zilizopita za mazungumzo ya kujaribu kuvimaliza vita vya Syria ambavyo vimedumu kwa zaidi ya miaka sita hazijaweza kufanikiwa kuutatua mzozo huo.

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Steffan Di Mistura alikutana jana na ujumbe wa serikali ya Syria na wa upinzani katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa.

Matumaini ya kuumaliza mzozo wa Syria ni madogo huku madai hayo kuwa maelfu ya wafungwa wanauawa na kisha kuchomwa katika gereza la Saydnaya yakizidisha uhasama kati ya pande mbili zinazozana.

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kukamilika mwishoni mwa wiki hii.

Vita vya Syria vimesababisha vifo vya zaidi ya watu laki tatu

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu