Watu karibu 22 wameuawa huko jamuhuri ya Afrika ya Kati.

In Kimataifa
Watu karibu 22 wameuawa katika muda wa siku tatu za mapigano huko Jamhuri ya Afrika ya Kati. Wafugaji wenye silaha walikabiliana na wapiganaji wanamgambo katika mji wa kusini mashariki kuanzia siku ya Jumatano na milio ya risasi imeendelea kusikika hadi jana Ijumaa.
Ingawa chanzo cha mapigano hayo hakijajulikana, lakini wafugaji waliohusika katika mapigano hayo wanaaminika kuwa na mahusiano na kundi moja lililokuwa chini ya muungano wa kiislamu wa Seleka ambao umesambaratishwa.
Kundi hilo ndilo lililomuondoa rais Francois Bozize madarakani mwaka 2013.
Tangu wakati huo, maelfu ya watu wamepoteza maisha na wengine wengi wakiyakimbia makazi yao.
Umoja wa Mataifa umekadiria kuwa karibu watu 1000 wamekimbia makazi yao kutoka mkoa huo wa kusini mashariki baada ya machafuko ya wiki hii.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu