Watu karibu 22 wameuawa huko jamuhuri ya Afrika ya Kati.

In Kimataifa
Watu karibu 22 wameuawa katika muda wa siku tatu za mapigano huko Jamhuri ya Afrika ya Kati. Wafugaji wenye silaha walikabiliana na wapiganaji wanamgambo katika mji wa kusini mashariki kuanzia siku ya Jumatano na milio ya risasi imeendelea kusikika hadi jana Ijumaa.
Ingawa chanzo cha mapigano hayo hakijajulikana, lakini wafugaji waliohusika katika mapigano hayo wanaaminika kuwa na mahusiano na kundi moja lililokuwa chini ya muungano wa kiislamu wa Seleka ambao umesambaratishwa.
Kundi hilo ndilo lililomuondoa rais Francois Bozize madarakani mwaka 2013.
Tangu wakati huo, maelfu ya watu wamepoteza maisha na wengine wengi wakiyakimbia makazi yao.
Umoja wa Mataifa umekadiria kuwa karibu watu 1000 wamekimbia makazi yao kutoka mkoa huo wa kusini mashariki baada ya machafuko ya wiki hii.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu