Watu karibu 22 wameuawa huko jamuhuri ya Afrika ya Kati.

In Kimataifa
Watu karibu 22 wameuawa katika muda wa siku tatu za mapigano huko Jamhuri ya Afrika ya Kati. Wafugaji wenye silaha walikabiliana na wapiganaji wanamgambo katika mji wa kusini mashariki kuanzia siku ya Jumatano na milio ya risasi imeendelea kusikika hadi jana Ijumaa.
Ingawa chanzo cha mapigano hayo hakijajulikana, lakini wafugaji waliohusika katika mapigano hayo wanaaminika kuwa na mahusiano na kundi moja lililokuwa chini ya muungano wa kiislamu wa Seleka ambao umesambaratishwa.
Kundi hilo ndilo lililomuondoa rais Francois Bozize madarakani mwaka 2013.
Tangu wakati huo, maelfu ya watu wamepoteza maisha na wengine wengi wakiyakimbia makazi yao.
Umoja wa Mataifa umekadiria kuwa karibu watu 1000 wamekimbia makazi yao kutoka mkoa huo wa kusini mashariki baada ya machafuko ya wiki hii.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu