Bobi Wine ashinda Ubunge.

In Kimataifa
Mwanamuziki mashuhuri wa mtindo wa Afrobeats nchini Uganda Ugandan Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo nchini humo.
Wine, ambaye aliwania kama mgombea huru, aliwashinda wagombea wengine wane katika eneo bunge la Kyadondo Mashariki katikati mwa Uganda.
Alipata kura elfu 25,659 kutoka kwa kura elfu 33,310 zilizopigwa, gazeti la serikali la New Vision limeripoti.
Gazeti hilo linasema baada ya kutangazwa mshindi, aliahidi kuangazia zaidi kuwaunganisha raia.
Mwanamuziki huyo alikuwa amekamatwa na polisi na kuhojiwa kwa muda kabla ya kuachiliwa siku chache zilizopita.
Kiti hicho cha ubunge kiliachwa wazi baada ya mahakama kuamua kuwa uchaguzi uliofanyika mapema mwaka jana haukufuata kanuni na sheria za uchaguzi.
Kiongozi wa chama cha upinzani cha FDC Kizza Besigye amempongeza mwanamuziki huyo kwenye Twitter.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu