Bobi Wine ashinda Ubunge.

In Kimataifa
Mwanamuziki mashuhuri wa mtindo wa Afrobeats nchini Uganda Ugandan Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo nchini humo.
Wine, ambaye aliwania kama mgombea huru, aliwashinda wagombea wengine wane katika eneo bunge la Kyadondo Mashariki katikati mwa Uganda.
Alipata kura elfu 25,659 kutoka kwa kura elfu 33,310 zilizopigwa, gazeti la serikali la New Vision limeripoti.
Gazeti hilo linasema baada ya kutangazwa mshindi, aliahidi kuangazia zaidi kuwaunganisha raia.
Mwanamuziki huyo alikuwa amekamatwa na polisi na kuhojiwa kwa muda kabla ya kuachiliwa siku chache zilizopita.
Kiti hicho cha ubunge kiliachwa wazi baada ya mahakama kuamua kuwa uchaguzi uliofanyika mapema mwaka jana haukufuata kanuni na sheria za uchaguzi.
Kiongozi wa chama cha upinzani cha FDC Kizza Besigye amempongeza mwanamuziki huyo kwenye Twitter.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu