Bobi Wine ashinda Ubunge.

In Kimataifa
Mwanamuziki mashuhuri wa mtindo wa Afrobeats nchini Uganda Ugandan Robert Kyagulanyi Ssentamu, maarufu kama Bobi Wine, ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo nchini humo.
Wine, ambaye aliwania kama mgombea huru, aliwashinda wagombea wengine wane katika eneo bunge la Kyadondo Mashariki katikati mwa Uganda.
Alipata kura elfu 25,659 kutoka kwa kura elfu 33,310 zilizopigwa, gazeti la serikali la New Vision limeripoti.
Gazeti hilo linasema baada ya kutangazwa mshindi, aliahidi kuangazia zaidi kuwaunganisha raia.
Mwanamuziki huyo alikuwa amekamatwa na polisi na kuhojiwa kwa muda kabla ya kuachiliwa siku chache zilizopita.
Kiti hicho cha ubunge kiliachwa wazi baada ya mahakama kuamua kuwa uchaguzi uliofanyika mapema mwaka jana haukufuata kanuni na sheria za uchaguzi.
Kiongozi wa chama cha upinzani cha FDC Kizza Besigye amempongeza mwanamuziki huyo kwenye Twitter.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Trump apiga marufuku raia wa mataifa 12 kuingia Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump ametia saini tangazo jipya linaloweka marufuku kali kwa raia wa mataifa 12 kuingia nchini

Read More...

Serikali Yafuta Usajili wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Linaloongozwa na Askofu Gwajima

Serikali kupitia Msajili wa Jumuiya za Kiraia, Emmanuel Kihampa, imetangaza kulifutia usajili Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na

Read More...

KATIBA YA CCM YAFANYIWA MABADILIKO 

Kwa mujibu wa taarifa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu