Ali Reza Akbari ahukumiwa kifo

In Kimataifa

Iran imemuhukumu kifo afisa mkuu wa zamani wa ulinzi baada kumkuta na hatia kwa mashtaka ya kuifanyia ujasusi Uingereza, chombo cha habari chenye uhusiano na serikali kimeripoti Jumatano.

Mahakama imesema Ali Reza Akbari, ambaye alikuwa naibu waziri wa ulinzi hadi mwaka 2001, alikuwa “jasusi mkuu” wa idara ya ujasusi ya Uingereza, shirika la habari la Tasmin limeripoti.

Tasmin imeripoti pia kuwa alifanya ujasusi kwenye mazungumzo ya zamani ya nyuklia kati ya Iran na mataifa ya magharibi.

Akbari alihudumu kama naibu waziri wa ulinzi chini ya uongozi wa Rais Mohammad Khatami, mwanamageuzi ambaye alishinikiza kuboreshwa kwa uhusiano na nchi za magharibi.

Uingereza imeomba hukumu hiyo isitishwe na Akbari aachiliwe mara moja.

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza James Cleverly amesema katika taarifa “ Hiki ni kitendo kilichochochewa kisiasa na utawala wa kikatili ambao unapuuza kabisa maisha ya binadamu.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu