Benki ya biashara Afrika ( CBA) yazindua huduma mpya ya kibenki, inayomwezesha mteja kuhudumiwa.

In Kitaifa, Uchumi

Benki  ya biashara  Afrika ( CBA)  imezindua huduma mpya  ya kibenki, inayomwezesha mteja kuhudumiwa

kibinafsi popote pale alipo, kwa kupewa vipaumbele tofauti badala ya kufuata huduma hiyo benki.

Aidha huduma hiyo ambayo ni tofauti inamsaidia mteja kupata huduma zote za kibenki kibinafsi, na kuondoa changamoto kubwa iliyokuwepo ya wateja kutoka mbali na kufuata huduma hiyo.

Akizungumza  wakati wa kuzindua huduma hiyo jijini Arusha, Mkurugenzi wa benki hiyo nchini Tanzania, Gift Shoko amesema kuwa, huduma hiyo itakuwa inafanya kazi katika mikoa ya Arusha, Dar es salaam, na Mwanza.

Shoko amesema kuwa, lengo la kuanzisha huduma hiyo, ni baada ya kugundua watu wengi wanakosa nafasi kutokana na majukum, kwa maendeleo ya nchi na kuwafanya kukosa muda wa kufika  benki , hivyo wameona umuhimu wa kuwafikia pale walipo, katika kupata huduma mbalimbali muhimu.

Mwenyekiti wa benki hiyo Ndewirwa  Kitomari , amesema kuwa, CBA  ndio benki ya kwanza kutoa mikopo ya nyumba, ambapo wamejiwekea mikakati ya kutoa mikopo ya riba nafuu kwa wajasiriamali huku wakijikita zaidi katika kukuza uchumi wa viwanda.

benki  ya CBA ambayo ilianzishwa mwaka 1962  ina jumla ya matawi 11 nchini, ambapo ipo pia katika nchi za Afrika mashariki ambazo ni Kenya, Uganda na Rwanda

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu