CAF Yaipa Morocco Ubingwa Baada ya Rufaa Kufuatia Utata wa Fainali

In Kimataifa, Michezo

Shirikisho la Soka barani Afrika, Confederation of African Football (CAF), limeitunuku Morocco ubingwa wa mashindano hayo kufuatia uamuzi wa bodi ya rufaa uliotolewa siku 58 baada ya mchezo wa fainali uliochezwa Januari 18 mjini Rabat, Morocco.

Awali, Senegal ilikuwa imetangazwa mshindi wa fainali hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Morocco katika mchezo uliokuwa na ushindani mkali. Hata hivyo, mechi hiyo iligubikwa na utata mkubwa baada ya wachezaji wa Senegal kususia kuendelea na mchezo wakipinga maamuzi ya mwamuzi, hususan kutolewa kwa mkwaju wa penalti katika dakika za mwisho wakati matokeo yakiwa 0-0.

Mchezo huo ulisimama kwa takribani dakika 17 huku hali ya taharuki ikitawala uwanjani. Baadaye, wachezaji wa Senegal walirejea uwanjani kuendelea na mchezo kufuatia juhudi za kuwashawishi zilizofanywa na mshambuliaji nyota Sadio Mané. Penalti ya Morocco iliyopigwa na Brahim Díaz iliokolewa na kipa Edouard Mendy kabla ya Senegal kufunga bao la ushindi kupitia Pape Gueye katika muda wa nyongeza.

Hata hivyo, baada ya mchezo huo, Morocco iliwasilisha rufaa kwa CAF ikipinga matukio yaliyojitokeza wakati wa mchezo. Katika uamuzi wake uliotolewa na bodi ya rufaa, CAF imebainisha kuwa Senegal ilikiuka kanuni za mashindano, na hivyo “inachukuliwa kuwa imepoteza mchezo huo kwa kufungwa mabao 3-0.”

Kutokana na uamuzi huo, Morocco imepewa ushindi rasmi wa mechi hiyo pamoja na ubingwa wa mashindano hayo. Aidha, CAF imetangaza adhabu mbalimbali, zikiwemo faini kwa pande zote mbili, huku baadhi ya hoja za rufaa za Morocco zikikubaliwa na nyingine kukataliwa.

Uamuzi huo umeibua mjadala mpana katika duru za soka, na unaingia katika historia kama mojawapo ya maamuzi yenye utata mkubwa kuwahi kufanywa katika soka la Afrika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu