RAIS SAMIA AMUASILI MTOTO MCHANGA ALIYETELEKEZWA NZEGA

In Kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amemuasili leo mtoto mchanga wa kike aliyepewa jina Grace Samia Suluhu, katika makazi yake, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma.

Mtoto huyo alitelekezwa mjini Nzega, mkoani Tabora, na amekabidhiwa kwa Rais Dkt. Samia na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Mhe. Naitapwaki Tukai. Akizungumza wakati wa kumkabidhi, Mkuu wa Wilaya Tukai alieleza kuwa mtoto huyo aliokotwa tarehe 17 Januari 2026 karibu na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega Mjini.

“Tarehe tuliopokea taarifa, tulishirikiana na Jeshi la Polisi kumchukua mtoto na kumpeleka hospitalini kwa uchunguzi na uangalizi maalum. Juhudi za kumtafuta mama yake zinaendelea bila mafanikio hadi sasa,” alisema Mkuu wa Wilaya.

Rais Dkt. Samia amemkaribisha mtoto huyo katika familia yake na kuahidi kumpatia malezi, ulinzi wa kisheria, na huduma zote muhimu za msingi, kuhakikisha akue katika mazingira salama, yenye upendo na maendeleo stahiki.

Rais Dkt. Samia pia alisisitiza umuhimu wa kutoa watoto waliotelekezwa kwa mamlaka husika

“Wanaotupa watoto hawajui wanalolifanya. Kuliko kumtupa mtoto ni bora kumkabidhi katika mamlaka za kisheria au kituo cha kulelea watoto. Kila mtoto aliyezaliwa ni hazina, na hatuwezi kujua kesho yake.”

Uamuzi huu unaashiria dhana ya Serikali ya kulinda haki za watoto, kuhakikisha usalama wao, na kutoa malezi bora kwa watoto wote walio hatarini.
#radio5fm

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Rais Samia Azungumza na Wananchi Dodoma Kabla ya Safari ya Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali ya

Read More...

Dkt. Samia Azungumza na Wajumbe wa Shina Na. 1 CCM Chamwino Dodoma

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan

Read More...

Marekani yaiona Tanzania kuwa mshirika muhimu kimkakati

Balozi mteule wa Marekani nchini Tanzania, William Trachman, amesema pamoja na changamoto zilizojitokeza baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025,

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu