CARDINAL PENGO AFARIKI DUNIA

In Kitaifa

Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki la Dar es Salaam limetangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo hilo. Kwa mujibu wa taarifa rasmi, Kardinali Pengo amefariki usiku wa kuamkia leo majira ya saa 4:00 akiwa amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), jijini Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu. Taarifa hiyo imetolewa na Askofu Mkuu wa Dar es Salaam, Thaddeus S. Ruwa’ichi, ambaye ameeleza kuwa ratiba na taratibu za mazishi zitatangazwa baadaye mara baada ya mipango kukamilika. Jimbo Kuu limewaomba waumini na watu wote wenye mapenzi mema kuendelea kuliombea Kanisa na kumuombea marehemu apate pumziko la milele.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu