MAMA YAKE CHID BENZ AFARIKI DUNIA.

In Burudani, Kitaifa

Mama wa msanii wa muziki wa Hip-hop nchini, Rashid Abdallah maarufu kama Chid Benz, Hawa Idd Mwamanda, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Februari 11, 2025, nyumbani kwake.

Akithibitisha taarifa za msiba huo, Chid Benz amesema kuwa kwa sasa msiba upo nyumbani kwao mtaa wa Masantula, Chanika jijini Dar es Salaam. Ameeleza kuwa wakati taarifa za kifo hicho zinamfikia alikuwa studio na anaelekea nyumbani kushiriki katika taratibu za awali za msiba.

Msanii huyo amesema amekuwa akipokea maswali mengi kuhusu mipango ya mazishi, lakini amesisitiza kuwa uamuzi rasmi utatolewa na kaka yake mkubwa baada ya familia kukamilisha mashauriano. Ameongeza kuwa ni vyema watu wakafika nyumbani kwa marehemu ili, endapo mazishi yatafanyika leo, waweze kushiriki pamoja na familia.

Taarifa rasmi kuhusu ratiba na taratibu za mazishi zinatarajiwa kutolewa baadaye na familia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu