Common ni mmoja kati ya marapa wazuri wa Hip Hop
kwenye game, na linapokuja suala la maswala kama mfumo wa
gereza na jinsi inavyoathiri maisha ya wamarekani weusi, rapa
huyo wa Chicago sio mtu wa kukaa kimya na kutazama mambo
yanavyotokea.
Jumanne (Oktoba 5), CBS Chicago iliripoti kuwa Common
alifungua studio ya kurekodi inayofanya kazi kikamilifu ndani ya
Kituo cha Marekebisho ya tabia cha Stateville huko Cresthill.
Mwanasheria Ari Williams mwanzoni alikuja na wazo la kuwapa
wafungwa wa Stateville fursa ya kutumia ubunifu wakati wa
kutumikia vifungo vyao.
Common alisema “wafungwa wanastahili kupata vitu bora
maishani kwa hivyo ndiyo sababu napigania jiji langu,” Common
alisema. “Na ndio sababu moyo wangu uko na Chicago kila
wakati.”
Common alisema katika interview. “Sababu ya kusema kwaajili
ya watu wengi ambao wamefungwa kwa sababu nimekuwa
nikienda kwenye magereza hayo na kukutana nao. Na sasa
naweza kusema kwa mtazamo mwingine kabisa, lakini ni
upendo. Sijali ikiwa haujafika bado kwenye mitaa na kujionea…
hivyo chimba kwa kina kidogo. Ni hayo tu.”



