Jamaa amuua mamake baada ya kukataa kumpa chakula.

In Kimataifa


Mwanaume mmoja mwenye miaka 25 anapatiwa matibabu
katika Hospitali ya Kyuso Level 4 kaunti Ndogo ya Mwingi
nchini Kenya kwa kula sumu, baada ya kumuua mama yake
mzazi mwenye miaka 58.


Kimanzi Muthui anaripotiwa kumchanachana Agnes Kisyinoi na
panga baada ya kukataa kumpa chakula cha jioni usiku wa
Jumatatu Mei 26 mwezi uliopita hapo.


Kulingana na polisi nchini humo mshukiwa aliwasali nyumbani
na kumuamuru mama yake ampakulie chakula lakini marehemu
alikataa na wakaanza kugombana.


Mshukiwa anasemekana alichukua panga na kumkata kata
mama yake mara kadhaa katika sehemu tofauti za mwili na
kusababisha kifo chake papo hapo.

Baada ya kufanya tukio hilo kijana huyo alikunywa sumu
akijaribu kijiua,lakini aliokolewa na majirani ambao
walimpeleka Hospitali.


Kwa sasa anakabiliwa na mashtaka mawili kwanza la mauaji ya
mama yake na la pili kutaka kujiuwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu