Kocha wa Hard Rock ataja sababu za kubamizwa na Simba.

In Kitaifa, Michezo

 

Baada ya kushuhudia timu yake ikiambulia kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Simba, Kocha wa timu ya Hard Rock, Muhibu Kanu amesema wachezaji wake walikuwa na hofu.

 

Kanu amesema mchezo huo umemsaidia kuona wapi ambapo kuna mapungufu katika kikosi chake, ambapo atayafanyia kazi lakini akadai kuwa wachezaji wake walikuwa na hofu kwa kuwa waliona wanacheza na timu kubwa.

 

Alidai kuwa ameona mapungufu na kwa kuwa ligi ya Zanzibar inatarajiwa kuanza hivi karibuni, anaamini Simba ilikuwa ni kipimo kizuri kwa wachezaji wake na benchi lao la ufundi limeshaona upungufu ulipo.

 

“Sijalia kufungwa kaisi kikubwa cha mabao, lakini naamini wachezaji wangu watakua wamejifunza kitu,na kwa upande wangu nimeona mapungufu yapo wapi, na ninaahidi nitayafanyia kazi ili kufanya maboresho.

 

“Wachezaji wangu walionyesha uoga dhidi ya wapinzani wao, na hii walijitengenezea mazingira ya kuogopa tangu mwanzo, kwa sababu ya jina la timu pinzani ya Simba, lakini bado hilo ni tatizo ambalo nimelibaini, nitalifanyia kazi ili kuwarejesha wachezaji katika saikolojia ya kupambana, na sio kuogopa jina”. Amesema Kanu

 

Mchezo wa jana ulikua wa kwanza kwa kocha Muhibu Kanu tangu alipomaliza masomo ya ukocha mkoani Morogoro, na anatarajia kukiongoza kikosi chake cha Hard Rock kwenye mshike mshike wa ligi ya Zanzibar ambao umepangwa kuanza Oktoba Mosi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu