Kocha wa Hard Rock ataja sababu za kubamizwa na Simba.

In Kitaifa, Michezo

 

Baada ya kushuhudia timu yake ikiambulia kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Simba, Kocha wa timu ya Hard Rock, Muhibu Kanu amesema wachezaji wake walikuwa na hofu.

 

Kanu amesema mchezo huo umemsaidia kuona wapi ambapo kuna mapungufu katika kikosi chake, ambapo atayafanyia kazi lakini akadai kuwa wachezaji wake walikuwa na hofu kwa kuwa waliona wanacheza na timu kubwa.

 

Alidai kuwa ameona mapungufu na kwa kuwa ligi ya Zanzibar inatarajiwa kuanza hivi karibuni, anaamini Simba ilikuwa ni kipimo kizuri kwa wachezaji wake na benchi lao la ufundi limeshaona upungufu ulipo.

 

“Sijalia kufungwa kaisi kikubwa cha mabao, lakini naamini wachezaji wangu watakua wamejifunza kitu,na kwa upande wangu nimeona mapungufu yapo wapi, na ninaahidi nitayafanyia kazi ili kufanya maboresho.

 

“Wachezaji wangu walionyesha uoga dhidi ya wapinzani wao, na hii walijitengenezea mazingira ya kuogopa tangu mwanzo, kwa sababu ya jina la timu pinzani ya Simba, lakini bado hilo ni tatizo ambalo nimelibaini, nitalifanyia kazi ili kuwarejesha wachezaji katika saikolojia ya kupambana, na sio kuogopa jina”. Amesema Kanu

 

Mchezo wa jana ulikua wa kwanza kwa kocha Muhibu Kanu tangu alipomaliza masomo ya ukocha mkoani Morogoro, na anatarajia kukiongoza kikosi chake cha Hard Rock kwenye mshike mshike wa ligi ya Zanzibar ambao umepangwa kuanza Oktoba Mosi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu