Sanchez aumia tena.

In Kimataifa, Michezo

Mshambuliaji Alexis Sanchez amethibitisha kukabiliwa na majeraha ya kifundo cha mguu, akiwa kwenye kambi ya timu yake ya taifa inayoendelea kusaka nafasi ya kucheza fainali za kombe la dunia za 2018 kule nchini Urusi.

Sanchez ametoa taarifa za kuumia, kupitia akaunti yake ya mtandao wa Instagram.

 

Mshambuliaji huyo amepatwa na majeraha hayo ikiwa ni baada ya kushuhudiwa akirejea uwanjani juma moja lililopita, katika mchezo wa ligi ya nchini England dhidi ya Liverpool, ambapo kikosi cha Arsenal kilikubali kuchapwa bakora nne kwa sifuri.

Tukio hilo la kuumia pia linatokea, baada ya usajili wa Sanchez kuelekea Man city kukwama dakika za mwisho kabla ya dirisha la usajili halijafungwa Agosti 31.

Sanchez alikosa michezo ya mwanzoni mwa msimu huu, kufuatia maumivu ya misuli ya tumbo ambayo yalimuweka nje kwa muda wa majuma mawili.

Sanchez alihusishwa na mipango ya kutaka kusajiliwa na Man city kwa kitita cha Pauni milioni 60, huku nafasi yake ilitajwa huenda ingezajwa na mshambuliaji wa pembeni wa AS Monaco Thomas Lemar ambaye thamani yake ilifikia Pauni milioni 92.

Bado haijafahamika Sanchez atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi gani, jambo ambalo huenda likaendelea kumuweka mashakani meneja wa Arsenal Arsene Wenger, ambaye anatamani kuendelea kumtumia, baada ya kugoma kumuuza.

Kwenye runinga moja nchini Ufaransa ya Telefoot, alisema alikuwa na ”sababu za kibinafsi” kutokana na uamuzi uliochelewa wa kuongeza muda wake wa miaka 21 na klabu hiyo.

Arsenal ilimaliza katika nafasi ya tano katika Ligi ya Premia msimu uliopita, ikiwa ni mara yao ya kwanza kumaliza chini ya nambari nne tangu Wenger alipojiunga na klabu hiyo mwaka 1996.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu