Tambwe, Chirwa wawatuliza yanga Jumamosi hii Njombe.

In Kitaifa, Michezo

Washambuliaji wa kutumainiwa wa Yanga, Obery Chirwa pamoja na Amissi Tambwe leo hii wataungana na kikosi hicho katika mazoezi ya kujiandaa na mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Njombe Mji katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Yanga na Njombe Mji zitapambana Jumamosi hii katika Uwanja wa Sabasaba mijini Njombe baada ya Shirikisho la Soka Tanzania kuifanyia mabadiliko ratiba ya ligi kuu ambapo awali ilikuwa zipambane Jumatano hii. Kitendo hicho cha nyota hao kujiunga na kikosi hicho kimepokelewa kwa mikono miwili na viongozi wa benchi la ufundi la timu hiyo baada ya kuwakosa kwa kipindi kirefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goti.

Majeraha hayo yaliwafanya wawe nje ya uwanja kwa kipindi kirefu huku wakishindwa kuitumikia timu yao hiyo katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba lakini pia ule wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Lipuli FC.

Mechi zote hizo Yanga haikufanya vizuri.Akizungumza na Championi Jumatatu, Daktari wa Yanga, Edward Bavu, alisema kuwa wachezaji hao kwa pamoja leo hii wataanza mazoezi baada ya kupona majeraha yao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu