Tambwe, Chirwa wawatuliza yanga Jumamosi hii Njombe.

In Kitaifa, Michezo

Washambuliaji wa kutumainiwa wa Yanga, Obery Chirwa pamoja na Amissi Tambwe leo hii wataungana na kikosi hicho katika mazoezi ya kujiandaa na mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Njombe Mji katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Yanga na Njombe Mji zitapambana Jumamosi hii katika Uwanja wa Sabasaba mijini Njombe baada ya Shirikisho la Soka Tanzania kuifanyia mabadiliko ratiba ya ligi kuu ambapo awali ilikuwa zipambane Jumatano hii. Kitendo hicho cha nyota hao kujiunga na kikosi hicho kimepokelewa kwa mikono miwili na viongozi wa benchi la ufundi la timu hiyo baada ya kuwakosa kwa kipindi kirefu kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goti.

Majeraha hayo yaliwafanya wawe nje ya uwanja kwa kipindi kirefu huku wakishindwa kuitumikia timu yao hiyo katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba lakini pia ule wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Lipuli FC.

Mechi zote hizo Yanga haikufanya vizuri.Akizungumza na Championi Jumatatu, Daktari wa Yanga, Edward Bavu, alisema kuwa wachezaji hao kwa pamoja leo hii wataanza mazoezi baada ya kupona majeraha yao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu