Mgombea Urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
Mh Tundu Lissu leo August 19 2020 akiwa Mkoani Mbeya
mjini akitafuta wadhamini amezungumza na wanambeya na
kusema watanzania wanahitaji mabadiliko makubwa kwani
watanzania hawataki tena wabunge wa CCM kulitawala bunge.
Katika taarifa ingine ni kwamba Kamanda wa Polisi mkoa wa
Kilimanjaro Emanuel Lukala, amesema mpaka sasa kuna watu 2
wanaoshikiliwa na jeshi hilo kutokana na vurugu alizofanyiwa
mgombea huyo wa Chadema kwa msafara wake kurushiwa
mawe na baadhi ya vijana aliowaita ni wahuni.



