Mahujaji 35 waaga dunia wakifanya ibada Makkah.

In Kimataifa

 

Katika Ibada ya Hijja inayofanyika kila mwaka na kutekelezwa na Waislamu nchini Saudi Arabia katika Msikiti Mkuu mji wa Makkah eneo takatifu, Mahujaji 35 wafariki dunia.

Taarifa hizo zimetolewa rasmi na Wizara ya Afya nchini Misri, ambapo imesema kuwa siku ya kwanza ya ibada hiyo imepoteza Mahujjaji 35 kutokana na sababu ya uchovu na umri mkubwa.

Afisa mmoja wa Wizara hiyo, Ahmed el Ansary, amesema umri wa Mahujaji waliofariki ni kati ya miaka 60 hadi 85.

Katika Ibada hiyo ya Hijja mwaka huu zaidi ya Mahujaji milioni mbili wamehudhuria wakiwemo milioni 1.8 kutoka nje ya nchi.

 

Mahujaji hao wamekuwa wakifanya utaratibu huo wakifuata nyayo za Mtume wao Muhammad, aliyefanya utaratibu huo wa ibada miaka 1400 iliyopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu