Njiwa aliyetumiwa kusafirisha mihadarati apigwa risasi.

In Kimataifa

Polisi nchini Argentina wamempiga risasi njiwa ambaye alitumiwa kusafirisha mihadarati kwenda gereza moja nchini humo, kwa mujibu wa mamlaka za gereza hilo.

Njiwa huyo alionekana akiruka hadi kwenye uwanja wa gereza hilo, lililo katika mji wa Santa Rosa.

Maafisa waligundua kuwa ndege huyo alikuwa amefungiwa mfuko mdogo kwenye mgongo wake, uliokuwa na vidonge vya madawa ya kulevya.

Njia hiyo ya kusafirisha madawa ilikuwa imegunduliwa, na ilikuwa ikifanyiwa uchunguzi.

Gazeti la Clarin lilichapisha picha ya njiwa huyo akiwa na mfuko mweupe, uliokuwa na tembe 44 za madawa ya kulevya.

Magereza nchini Argentina yalionya mwaka 2013 kuwa, walanguzi wa madawa ya kulevya walikuwa wakitumia njiwa waliokuwa wakifanya safari mara 10 hadi 15 kwa siku.

Watu watatu walikamatwa na njiwa 15 kupatikana, baada ya uchunguzi wa mwaka 2013.

Mapema mwaka huu njiwa ambaye alikuwa na mfuko uliokuwa na tembe 178 za dawa ya kulevya, alishikwa nchini Kuwait karibu na mpaka na Iraq.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu