Arsene Wenger asema ‘alisita’ kutia saini mkataba mpya Arsenal.

In Kimataifa, Michezo

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema ”alisita” wakati wa kutia saini mkataba mpya mwishoni mwa msimu uliopita kwa sababu hakuwa na uhakika kwamba ”angeweza kuiongoza klabu hiyo.”

Wenger alikubali mkataba wa miaka miwili mwezi Mei, mwezi mmoja kabla ya mkataba wake kumalizika.

Kwenye runinga moja nchini Ufaransa ya Telefoot, alisema alikuwa na ”sababu za kibinafsi” kutokana na uamuzi uliochelewa wa kuongeza muda wake wa miaka 21 na klabu hiyo.

Arsenal ilimaliza katika nafasi ya tano katika Ligi ya Premia msimu uliopita, ikiwa ni mara yao ya kwanza kumaliza chini ya nambari nne tangu Wenger alipojiunga na klabu hiyo mwaka 1996.

Arsenal walianza michuano ya msimu huu ya Ligi Kuu ya England kwa ushindi wa nyumbani wa magoli 4-3 dhidi ya Leicester,kabla kupoteza kwa Stoke kwa goli 1-0 na Liverpool 4-0.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu