MAMA YAKE CHID BENZ AFARIKI DUNIA.

In Burudani, Kitaifa

Mama wa msanii wa muziki wa Hip-hop nchini, Rashid Abdallah maarufu kama Chid Benz, Hawa Idd Mwamanda, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Februari 11, 2025, nyumbani kwake.

Akithibitisha taarifa za msiba huo, Chid Benz amesema kuwa kwa sasa msiba upo nyumbani kwao mtaa wa Masantula, Chanika jijini Dar es Salaam. Ameeleza kuwa wakati taarifa za kifo hicho zinamfikia alikuwa studio na anaelekea nyumbani kushiriki katika taratibu za awali za msiba.

Msanii huyo amesema amekuwa akipokea maswali mengi kuhusu mipango ya mazishi, lakini amesisitiza kuwa uamuzi rasmi utatolewa na kaka yake mkubwa baada ya familia kukamilisha mashauriano. Ameongeza kuwa ni vyema watu wakafika nyumbani kwa marehemu ili, endapo mazishi yatafanyika leo, waweze kushiriki pamoja na familia.

Taarifa rasmi kuhusu ratiba na taratibu za mazishi zinatarajiwa kutolewa baadaye na familia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAVUNDE ATOA MAAGIZO KWA MAOFISA MADINI

Waziri wa Madini, Antony Mavunde ametoa maagizo mbalimbali ikiwemo kuwataka Maofisa Madini Wakazi wa Mikoa nchini kumpa taarifa ya

Read More...

JTK YATOA WITO KWA VIJANA KUJIUNGA NA MAFUNZO.

MKUU wa Jeshi la kujenga Taifa,(JKT)Meja Jenerali RAJABU MABELE,,ametoa wito kwa Vijana wote wa Tanzania Bara na Visiwani kujiunga

Read More...

CCM YAONYA KAULI ZINAZOPOTOSHA UKWELI.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeonya dhidi ya kauli na mienendo inayopotosha ukweli kuchafua historia ya Taifa na kuhujumu amani

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu