Mamlaka ya Mapato TRA yakusanya shilingi trilioni 10.87 ndani ya miezi 9

In Kitaifa

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa ripoti ya mapato yaliyokusanywa ndani ya miezi 9 kuanzia June 2016 hadi March 2017 ambayo ni Shilingi Trilioni 10.87 ikiwa ni ongezeko la asilimia 9.99 ukilinganisha na mwaka uliopita.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo

Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo alisema zaidi ya Shilingi Trilioni 1.34 zilikusanywa katika mwezi March 2017 pekee ikionesha kupanda kwa asilimia 2.23 ukilinganisha makusanyo ya mwezi kama huo mwaka 2016 ambapo zilikusanywa Shilingi Trilioni” 1.31.

“Katika kipindi cha miezi 9 ambayo imeanzia mwezi wa June 2016 hadi mwezi Marchi 2017, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi Trilioni 10.87 za Kitanzania hayo ni makusanyo ya miezi tisa,”alisema Kayombo.

Aliendelea kufafanua kuwa, “Katika mwezi wa Machi 2017 TRA imekusanya jumla ya shilingi trilioni 1.34 ukilinganisha trilioni 1.31 ya mwezi machi 2016 ambayo ni sawa na aslimia 2.23. Pamoja na mafanikio tuliyoyapata katika kipindi cha miezi tisa iliyopita, katika kipindi cha miezi mitatu kilichobaki TRA itahakikisha inakusanya kodi mbalimbali ili kufikia lengo la kukusanya trilioni 15.1 kwa mwaka.”

Aidha Katika hatua nyingine, Kayombo amesema TRA inaendelea na mpango wake wa kukusanya kodi za majengo kwa kutoa viwango maalumu vya kodi kwa majengo ambayo bado hayajafanyiwa tathimini.

NINI MAONI YAKO???? COMMENT HAPA CHINI

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu