Mamlaka ya Mapato TRA yakusanya shilingi trilioni 10.87 ndani ya miezi 9

In Kitaifa

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa ripoti ya mapato yaliyokusanywa ndani ya miezi 9 kuanzia June 2016 hadi March 2017 ambayo ni Shilingi Trilioni 10.87 ikiwa ni ongezeko la asilimia 9.99 ukilinganisha na mwaka uliopita.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo

Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo alisema zaidi ya Shilingi Trilioni 1.34 zilikusanywa katika mwezi March 2017 pekee ikionesha kupanda kwa asilimia 2.23 ukilinganisha makusanyo ya mwezi kama huo mwaka 2016 ambapo zilikusanywa Shilingi Trilioni” 1.31.

“Katika kipindi cha miezi 9 ambayo imeanzia mwezi wa June 2016 hadi mwezi Marchi 2017, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi Trilioni 10.87 za Kitanzania hayo ni makusanyo ya miezi tisa,”alisema Kayombo.

Aliendelea kufafanua kuwa, “Katika mwezi wa Machi 2017 TRA imekusanya jumla ya shilingi trilioni 1.34 ukilinganisha trilioni 1.31 ya mwezi machi 2016 ambayo ni sawa na aslimia 2.23. Pamoja na mafanikio tuliyoyapata katika kipindi cha miezi tisa iliyopita, katika kipindi cha miezi mitatu kilichobaki TRA itahakikisha inakusanya kodi mbalimbali ili kufikia lengo la kukusanya trilioni 15.1 kwa mwaka.”

Aidha Katika hatua nyingine, Kayombo amesema TRA inaendelea na mpango wake wa kukusanya kodi za majengo kwa kutoa viwango maalumu vya kodi kwa majengo ambayo bado hayajafanyiwa tathimini.

NINI MAONI YAKO???? COMMENT HAPA CHINI

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu