Mkuu wa Mkoa wa Pwani akagua Maendeleo ya Mradi Sukari

In Kitaifa

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, alhaj Abubakar Kunenge ,amekagua
Maendeleo ya Mradi Sukari (Kilimo cha Muwa na Kiwanda cha
Sukari  CAKaha Lake Agro Investment Ltd) kilichopo Utete
Wilayani Rufiji ,unaotarajia kuzalisha Tani100,000 za sukari
kuondoa Nakisi ya sukari kwa nchi na nyingine kuuza nje ya
Nchi. 


Akizungumza akiwa Eneo la Mradi Kunenge ameeleza
wawekezaji hao wapo kwenye matayarisho  ya Uwekezaji  na
kuwa Eneo hilo lina ukubwa wa Hekta 15 ambalo lote litakuwa
kwa ajili ya Kilimo cha miwa .


Amesema wawekezaji hao tayari wamejenga njia ya umeme
iliyogharimu zaidi ya Shilingi Milioni 100 na Barabara
inajengwa na Matarajio ya Mkoa na Serikali  kwa Mradi huo ni
kupata Kodi,na Ajira ya watu zaidi 18,000.


Naye Mwakilishi wa Kampuni ya Lake Agro Investment
Abubakar Nassor amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan
kwa Mazingira mazuri ya Uwekezaji na Ushirikiano wanaoupata
kutoka Uongozi wa Mkoa. 
Ametoa Wito kwa Wananchi kuchangamkia Fursa hiyo  kwa
Kushiriki kwenye uchumi huo kwa kulima Miwa  kwa wale
wakulima wa Nje (Out growers) Wafanyabiashara kuleta
huduma na kujipatia kipato.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu