Mshauri wa usalama wa Trump kujiuzulu

In Kimataifa

Naibu mshauri wa maswala ya usalama wa rais wa Marekani Donald Trump ameombwa na serikali hiyo ajiuzulu baada ya miezi mitatu pekee ya uteuzi wake kulingana na vyombo vya habari vya Marekani.

Mc Farland ambaye aliwahi kuhudumu kama mchanganuzi wa kituo cha habari cha Fox News ametakiwa kuhudumu kama balozi wa Singapore badala yake kulingana na Bloomberg na Reuters.

Hatua hiyo inajiri baada ya Trump kumuondoa afisa wa mipango Steve Bannon katika baraza la usalama la taifa hilo.
Baraza hilo humshauri rais kuhusu maswala ya usalama wa kitaifa pamoja na maswala ya kigeni.

Uteuzi wa Banon mwezi Januari ulizua hofu kwamba swala la washauri wakuu lilikuwa likiingiziwa siasa.

Wachanganuzi wanasema kuwa hatua hiyo ya hivi karibuni inaonyesha kuwa mshauri mpya wa rais Trump kuhusu maswala ya usalama Luteni Jenerali McMaster analifanyia mabadiliko baraza hilo la NSC liliteuliwa na mtangulizi wake.

Aliyekuwa mshauri wa maswala ya usalama Luteni Jenerali Michael Flynn alifutwa kazi baada ya wiki tatu na siku tatu pekee, baada ya kubainika alimdanganya makamu wa rais kuhusu mazungumzo yake na balozi wa Urusi nchini Marekani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu