Watu 6,529 Wamefariki kwa ajali za Bodaboda Nchini

In Kitaifa

Bado Ajali za Bodaboda ni Kisababishi cha Maelfu ya Vifo Nchini.

Serikali imesema watu 6,529 wamefariki dunia huku watu 30,661 wakiwa wamejeruhiwa kutokana na ajali 31,928 zilizosababishwa na pikipiki maarufu bodaboda na bajaji katika kipindi cha miaka saba kati ya Januari 2010 hadi Februari 2017

Akijibu swali la mbunge Abdallah Haji Ali wa jimbo la Kiwani, aliyeuliza ni watu wangapi wamepoteza maisha na wangapi wamejeruhiwa kwa ajali za bodaboda kuanzia mwaka 2010 hadi 2017.

Waziri wa mambo ya ndani, mheshimiwa Mwigulu Nchemba, amesema usafiri wa bodaboda na bajaji ulianza mwaka 2008, lakini serikali ilipitisha kanuni na masharti ya usafirishaji mwaka 2010, lakini hakuwa na utaratibu wa kusimamia biashara hiyo.

Mheshimiwa Nchemba amesema kipindi cha Januari 2010 hadi Februari 2017, kumekuwa na jumla ya ajali 31,928 zilizosababisha vifo vya watu 6,529 na majeruhi 30,661.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu