Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia
Suluhu Hassan,leo alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya
siku ya kumbukumbu ya mashujaa yaliyofanyika jiini Dodoma.
Akizugumza katika Maadhimisho hayo yaliyofanyika leo Julai
25 2022,amewaambia watanzania ataendelea kuenzi mawazo ya
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na uamuzi wa Hayati
Dk John Magufuli,wa kuhamishia Serikali Dodoma akisema
kuwa hakuna kurudi nyuma.
Kwa upande mwingine Rais Samia amewakumbusha watanzania
kuendelea kuchanja chanjo ya Uviko 19,na pia kujiandikisha
kwenye zoezi la Sensa ya watu na makazi ambayo itafanyika
Agost 23.