Serikali ya Marekani kupitia Waziri wa mambo ya Nje Rex Tillerson, imetangaza kwamba itawawekea vikwazo washirika wa kibiashara wa Korea Kaskazini. Marekani imeendelea kuionya Korea Kaskazini kufuatia mpango wake wa kurusha makombora ya masafa marefu.

In Kimataifa
Serikali ya Marekani kupitia Waziri wa mambo ya Nje Rex Tillerson, imetangaza kwamba itawawekea vikwazo washirika wa kibiashara wa Korea Kaskazini. Marekani imeendelea kuionya Korea Kaskazini kufuatia mpango wake wa kurusha makombora ya masafa marefu.
Marekani imeamua kuiwekea shinikizo zaidi Korea Kaskazini kutokana na mpango wake wa nuklia na kuendelea kurusha makombora ya masafa marefu na kuishtumu nchi hiyo kuhatarish ausalama wa dunia.
Rex Tillerson amesisitiza kuwa Ikulu ya White House hivi karibuni itaamua ikiwa itaziwekea vikwazo nchi hizo.
Rex Tillerson alitoa onyo hili wakati wa kikao cha bunge kuhusu mahusiano ya ya kigeni siku ya Jumanne Juni 13.
Inasemekana kuwa Korea Kaskazini imepiga hatua katika kuunda makombora ya masafa marefu yenye uwezo wa kufika nchini Marekani.
Umoja wa Mataifa umeendelea kuishtumu Korea Kaskazini kufuatia majaribio yake ya makombora ya hivi karibuni.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu