Tanzania na Singapore: Miaka 45 ya urafiki

In Kitaifa

Tanzania na Singapore ni marafiki wa muda mrefu na mwaka huu wanasherehekea miaka 45 ya uhusiano wa kidiplomasia.

Uhusiano huu si wa kihistoria pekee, bali pia umejikita katika ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo ya kijamii.

Kwa sasa, Singapore imewekeza miradi 36 nchini Tanzania yenye thamani ya Dola milioni 535.13 za Marekani na imezalisha ajira 3,228 kwa Watanzania. Sekta zinazoguswa ni kilimo, usafirishaji, ujenzi, na rasilimali za asili.

Ziara ya siku tatu ya Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, kwa mwaliko wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, inalenga kuimarisha zaidi maeneo ya ushirikiano.

Wakuu hao watajadili biashara na uwekezaji, maendeleo ya bandari na usafirishaji, uchumi wa kidijitali, elimu na mafunzo ya ujuzi, utalii, miundombinu, teknolojia na ubunifu, pamoja na maendeleo endelevu.

Uhusiano huu unatarajiwa kuendelea kuimarika, na kuleta fursa zaidi za uwekezaji, ajira, na maendeleo ya miundombinu. Kwa Watanzania, hii ni nafasi ya kushiriki katika uchumi wa kidijitali na kujiweka katika ramani ya kimataifa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JKT yawaita wahitimu Form 6 2026 kujiunga na mafunzo ya lazima

Jeshi la Kujenga Taifa limewataka vijana wote waliohitimu kidato cha sita mwaka 2026 kutoka shule zote za Tanzania

Read More...

Arsenal Hatimaye Watwaa Taji la Premier League Baada ya Miaka 22 ya KusubiriNa Semio Sonyo – Radio 5

Klabu ya Arsenal hatimaye imeandika historia mpya kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England (Premier League) baada ya kusubiri

Read More...

TANROADS YAJENGA KM 243 ZA BARABARA ZA LAMI NDANI YA MIEZI 10

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) imeendelea kuimarisha sekta ya miundombinu nchini

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu