Taifa la Tanzania leo limeungana na Mataifa mengine barani
Afrika katika kuiadhimisha siku ya mtoto wa Afrika,ambapo
kitaifa imefanyika jijini Dodoma.
Kama huukuwa ukifahamu ni kwamba kunako Mwaka 1991
Wakuu wa OAU walianzisha Siku ya Mtoto wa Afrika kama
kumbukumbu ya uasi dhidi ya wanafunzi uliotokea hapo tarehe
16 Juni 1976 huko Soweto, Afrika Kusini.
Wakati huo wanafunzi waliandamana kupinga mfumo na elimu
Duni waliokuwa wanapatiwa,pili waliitaka Serikali ya kibaguzi
ya Afrika ya Kusini kuboresha mfumo wa lugha ya kufundishia.
Katika kuiadhimisha siku hii hapa nchini mgeni rasmi alikuwa
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wanawake na Makundi
Maalum Dkt Doroth Gwajima,na katika hotuba yake mbali ya
mambo mengine amezungumza adhma ya serikali kurekebisha
tena sera ya mtoto ili kuwalinda na vitendo vya unyanyasaji.



