Tume ya Taifa NEC yadadavua Taarifa Za Wagombea Ubunge Na Udiwani Kupita Bila Kupingwa

In Kitaifa

Tume  ya taifa ya uchaguzi (NEC) leo Agosti 26, imezungumza na wanahabari kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo uchaguzi, ambapo kubwa zaidi wametoa rai kwa vyombo vya habari kufanya kazi zao kwa weledi zaidi katika kipindi hiki cha uchaguzi.


Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera amesema, hadi kufikia 6:32 mchana, tume hiyo ilikuwa haijapokea pingamizi lolote la nafasi ya urais. Mwisho wa kuweka pingamizi ni saa 10 jioni.


“Agosti 25,2020 tume ilikamilisha uteuzi wagombea urais na makamu, ubunge na udiwani, hatujatoa taarifa yoyote juu ya zoezi hili, tayari vyombo vya habari kadhaa vinaaza kutoa matokeo ya uteuzi huu, hii ni kinyume na sheria.
”Unapotangaza mtu amepita bila kupingwa hiyo inaweza pelekea uvunjifu wa amani pale mtu anapowekewa mapingamizi, isionekane ameshinda. Mimi mwenyewe mkurugenzi wa uchaguzi sijapata majina hayo rasmi.


”Kumekuwepo na dhana ambayo wanadhani watu wanakatwa, suala la uteuzi huwezi kukata mtu kwa matakwa yako, sababu tume inafanya kazi kwa kuzingatia kanuni, tumeweka masharti ya uteuzi kwa urais wa Tanzania, ubunge na udiwani.


“Unapowekea mtu pingamizi au ukiona hakuteuliwa maana yake hajatekeleza masharti, mtu akitoa maneno nje ya masharti hatafanikiwa sababau huyu akitaka rufaa atashinda. Tume inafanya kazi kwa uwazi na uhuru,” amesema Dkt. Mahera.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu