Ukraine iko tayari kwa mazungumzo na Russia.

In Kimataifa

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema kwamba yupo tayari kwa mazungumzo na Russia, lakini iwapo tu mazungumzo hayo yatakuwa ya kweli na yenye kuhakikisha kwamba Ukraine inarejeshewa mipaka yake na kuheshimiwa.

Mazungumzo hayo vile vile yanastahili kupatia Ukraine fidhia kutokana na mashambulizi ya Russia na kuwachukulia hatua kali wahusika katika uhalifu wa vita nchini humo.

Zelenskiy amesema hayo katika hotuba yake ya jumatatu usiku, siku moja baada ya gazeti la Washington post kuripoti kwamba Marekani inataka Ukraine kuonyesha dalili za kutaka mazungumzo yafanyike.

Washington post liliripoti kwamba hatua ya Marekani kutaka Ukraine kufanya mazungumzo na Russia ni ya kimkakati ili kuendelea kupata msaada kutoka kwa washirika wake.

Katika hotuba hiyo ambayo ameitoa kabla ya kuhutubia kongamano kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, Zelenskiy amesema kwamba mtu yeyote ambaye ana dhamira ya kweli kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, anastahili kuonyesha kwamba anajali sana kuhusu nia ya kukomesha vita vinavyoendelea Ukraine.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu