Ukraine iko tayari kwa mazungumzo na Russia.

In Kimataifa

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema kwamba yupo tayari kwa mazungumzo na Russia, lakini iwapo tu mazungumzo hayo yatakuwa ya kweli na yenye kuhakikisha kwamba Ukraine inarejeshewa mipaka yake na kuheshimiwa.

Mazungumzo hayo vile vile yanastahili kupatia Ukraine fidhia kutokana na mashambulizi ya Russia na kuwachukulia hatua kali wahusika katika uhalifu wa vita nchini humo.

Zelenskiy amesema hayo katika hotuba yake ya jumatatu usiku, siku moja baada ya gazeti la Washington post kuripoti kwamba Marekani inataka Ukraine kuonyesha dalili za kutaka mazungumzo yafanyike.

Washington post liliripoti kwamba hatua ya Marekani kutaka Ukraine kufanya mazungumzo na Russia ni ya kimkakati ili kuendelea kupata msaada kutoka kwa washirika wake.

Katika hotuba hiyo ambayo ameitoa kabla ya kuhutubia kongamano kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, Zelenskiy amesema kwamba mtu yeyote ambaye ana dhamira ya kweli kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, anastahili kuonyesha kwamba anajali sana kuhusu nia ya kukomesha vita vinavyoendelea Ukraine.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu