Viongozi wa Afrika Mashariki kutuma Jeshi Congo

In Kimataifa

Viongozi wa Afrika Mashariki wamekubaliana jana Jumatatu
kutuma jeshi la kikanda mashariki mwa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo na kutoa mwito wa mapigano
kusitishwa mara moja.


Hatua hiyo ilitangazwa aa ofisi ya rais wa Kenya Uhuru
Kenyatta baada ya wakuu wa mataifa saba ya Jumuiya ya Afrika

Mashariki kufanya mazungumzo mjini Nairobi kuhusiana na
kuongezeka kwa machafuko mashariki mwa Kongo.


Kulingana na ofisi hiyo ya rais Uhuru Kenyatta, wakuu hao
wameliagiza jeshi hilo la kikanda kushirikiana na vikosi vya
Kongo kurejesha utulivu na kuhakikisha amani inapatikana.


Hata hivyo taarifa hiyo haikusema iwapo Rwanda inayolaumiwa
kuwasaidia waasi itaunganishwa kwenye jeshi hilo, ingawa
serikali ya Kongo inasisitiza haitakubali wanajeshi hao
kujumuishwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu