Wafanyakazi 22 wa UN raia wa Ethiopia Wanashikiliwa na Serikali Addis Ababa

In Kimataifa

Umoja wa mataifa Jumanne umesema kwamba wafanyakazi wake 22 raia wa Ethiopia walishikiliwa na serekali kuu ya Ethiopia mjini Addis Ababa, kufuatia uvamizi ulioripotiwa kuwalenga Wa-Tigray.

Wafanyakazi sita wa Umoja wa Mataifa wameachiliwa.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, amewaeleza wanahabari kwamba wafanyakazi 16 bado wanashikiliwa, na wanafanyakazi na serekali ya Ethiopia moja kwa moja kuhakikisha wanaachiliwa.

Amesema hakuna maelezo yaliyo tolewa juu ya sababu ya kushikiliwa kwa wafanyakakazi hao ambao wanafanyakazi katika idara mbalimbali.

Amesema baadhi yao wameshikiliwa toka siku kadhaa zilizopita.

Maafisa wa usalama wa Umoja wa Mataifa wamewatembelea wafanyakazi hao walio shikiliwa.

Septemba 30 serekali ya Ethiopia iliwafukuza wafanyakazi saba wa Umoja wa Mataifa wanaofanyakazi katika idara ya misaada ya kibinadamu, na kusema walikuwa wanaingilia masuala ya ndani ya Ethiopia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu