Wakili ataka kesi ya ubakaji inayomkabili JAY Z ifutwe

In Kimataifa

Wakili wa Jay-Z, Alex Spiro, ameendelea kupinga vikali kesi ya madai inayomkabili mteja wake, akibainisha kutokuwepo kwa uthibitisho wa msingi na kueleza mapungufu makubwa katika simulizi ya mshtaki. Haya yanakuja baada ya mshtaki, anayejulikana kama “Jane Doe,” kufichua baadhi ya madai yake kuhusu tukio la unyanyasaji wa kijinsia lililotokea miaka 24 iliyopita.

Katika mahojiano ya kituo kimoja cha runinga, mshtaki alitoa maelezo yaliyoibua maswali zaidi. Mwanamke huyo alisema baba yake alimchukua baada ya unyanyasaji huo, lakini pia alidai kutokumbuka tukio hilo vizuri. Aidha, alidai kuwa alizungumza na mtu mashuhuri kwenye hafla baada ya sherehe aliposema alishambuliwa, lakini mtu huyo mashuhuri alisema hakuwa New York wakati huo. Zaidi ya hayo, picha za jioni hiyo zinaonyesha Jay-Z na Sean “Diddy” Combs wakiwa katika eneo tofauti na lile alilotaja.

Jay-Z alitoa taarifa kupitia runinga siku ya Ijumaa, akisisitiza kwamba:

“Tukio hili halikutokea, na bado limewasilishwa mahakamani na kuenezwa mara mbili kwenye vyombo vya habari.”

Wakili Alex Spiro amesisitiza kwamba kesi hiyo inapaswa kufutwa haraka na jina la Jay-Z kusafishwa, huku akieleza kuwa tuhuma hizi ni za uongo na zinalenga kumharibia sifa msanii huyo maarufu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu