Waziri wa nchi ofisi ya rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa TAMISEMI Selemani Jafo, ametoa wito kwa wanafunzi
waliokosa nafasi za kujiunga na masomo ya kidato cha tano kwa
kukosa tahasusi zinazokidhi vigezo.
Wanafunzi hao wametakiwa kuomba nafasi za masomo katika
vyuo vinavyosimamiwa na NACTE ili kuweza kupata nafasi ya
kuendelea na masomo katika vyuo hivyo.
Jafo ametoa wito huo jijini Dodoma wakati akitoa taarifa kuhusu
matokeo ya uchaguzi wa awamu ya pili ya wanafunzi
waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano.