Watu 29 wamejeruhiwa baada ya lori kugonga treni jijini Dodoma jana majira ya saa 5.30 usiku.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Protas Katambi,amesema ametoa maagizo kwa vyombo vya usalama kumsaka dereva wa lori ambaye inasemekana aliruka kutoka kwenye lori, baada ya ajali hiyo kisha kutokomea kusikojulikana.
Shughuli ya kuondoa mabehewa ya treni inaendelea huku ulinzi ukiwa umeimarishwa katika eneo la tukio huku polisi waliokuwa na silaha wakiwa wameimarisha ulinzi katika tukio.
Kwa upande wake Kamanda wa Mkoa wa Dodoma Kamanda Gilles Muruto amezungumzia juu ya ajali hiyo pamoja na hali ya majeruhi wa ajali hiyo.