Watu takribani 700 wauawa Nchini Ethiopia.

In Kimataifa

Tume ya haki za binadamu nchini Ethiopia imesema kuwa watu takribani 700 wameuawa mnamo miezi 16 iliyopita kutokana na ghasia zilizoibuka nchini humo.
Uchunguzi wa tume hiyo umebainisha kuwa wengi wao waliuawa wakati wa maandamano, pale polisi walipotumia nguvu kuzima vuguvugu la upinzani lililoshamiri katika maeneo ya vijijini mwaka mmoja uliopita.
Watu wa jamii ya Oromo waliandamana katika jimbo lao na pia katika mji mkuu, Addis Ababa, wakilalamikia kutengwa katika shughuli za kisiasa na za kiuchumi. Sheria ya hali ya hatari ya miezi sita ilitangazwa mwezi Oktoba nchini Ethiopia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu