Makamu wa Rais wa Marekani na naibu Waziri mkuu wa Japan wakubaliana kuweka msukumo wa kidiplomasia na kiuchumi dhidi ya Korea Kaskazini.

In Kimataifa

Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence na naibu Waziri mkuu wa Japan Taro Aso,wamekubaliana kuweka msukumo wa Kidiplomasia na kiuchumi dhidi ya Korea Kasikazini kuishinikiza kuachana na mpango wake wa silaha za Nyuklia.
Akizungumza mjini Tokyo Japan, Pence amesema Marekani ina amini kuwa njia yenye mafanikio ni mazungumzo ya kimataifa kuishinikiza na kuitenga Korea Kaskazini kutokana na msimamo wake,lakini amesisitiza kuwa njia zote zina uzito wake.
Marekani itaendelea kushirikiana na Japan na washirika wengine katika ukanda na China,kuweka vikwazo vya kidplomasia na kiuchumi dhidi ya Korea Kaskazini,ili iachane na mpango wake wa silaha za nyuklia.Lakini mapendekezo yote yanaendelea kujadiliwa.
Katika mkutano huo Abe amemwambia Pence kuwa Japan inataka kufikia makubaliano kwa njia ya majadiliano.
Marekani kwa sasa imekuwa ikitafutwa uungwaji mkono katika kuikabili Korea Kaskazini.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu