Makamu wa Rais wa Marekani na naibu Waziri mkuu wa Japan wakubaliana kuweka msukumo wa kidiplomasia na kiuchumi dhidi ya Korea Kaskazini.

In Kimataifa

Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence na naibu Waziri mkuu wa Japan Taro Aso,wamekubaliana kuweka msukumo wa Kidiplomasia na kiuchumi dhidi ya Korea Kasikazini kuishinikiza kuachana na mpango wake wa silaha za Nyuklia.
Akizungumza mjini Tokyo Japan, Pence amesema Marekani ina amini kuwa njia yenye mafanikio ni mazungumzo ya kimataifa kuishinikiza na kuitenga Korea Kaskazini kutokana na msimamo wake,lakini amesisitiza kuwa njia zote zina uzito wake.
Marekani itaendelea kushirikiana na Japan na washirika wengine katika ukanda na China,kuweka vikwazo vya kidplomasia na kiuchumi dhidi ya Korea Kaskazini,ili iachane na mpango wake wa silaha za nyuklia.Lakini mapendekezo yote yanaendelea kujadiliwa.
Katika mkutano huo Abe amemwambia Pence kuwa Japan inataka kufikia makubaliano kwa njia ya majadiliano.
Marekani kwa sasa imekuwa ikitafutwa uungwaji mkono katika kuikabili Korea Kaskazini.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu