Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma Mh Deogratius Ndejembi,amesema watumishi wa umma
wapatao Elfu moja mia nne sabaini na saba,wamesimamishwa
kazi kwa kukiuka sheria, kanuni, taratibu na miongozo
inayosimamia nidhamu katika utumishi wa umma.
Ndejembi ameyasema hayo leo Bungeni jijini Dodoma,wakati
akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mlimba CCM Godwin
Kunambi.
Mbunge Kunambi aliuliza namna mashauri yanayoendelea
kusikilizwa na Tume ya Utumishi wa Umma yanachukua muda
mrefu sana.



