Imeelezwa kuwa suala la Kumlinda Mtoto ni Wajibu wa kila mmoja katika Eneo lolote alipo ili kuhakikisha Taifa linakuwa bora na kutengeneza Viongozi wajao.
Kauli hiyo imetolewa na Mtaalamu wa jinsia na Utetezi kutoka Shirika la World Vission Tanzania Bi. Tumain Fredy wakati akizungumza kulekea Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo huadhimishwa June 16 ya kila Mwaka.
Bi, Tumain amesema suala la kumlinda Mtoto ni Jukumu la kila mmoja bila kujali huyo ni Mtoto wa nani.
Katika hatua nyingine amesema WORLD VISSION wameamua kushirikiana na Viongozi wa Dini katika kupambana kulinda haki ya Mtoto kwa sababu Viongozi hoa wana uwanda mpana wa kukutana na Jamii.