Zelensky aionya Urusi, Itaongeza mashambulizi

In Kimataifa

Rais wa ukraine Volodymyr Zelensky ameonya jana kwamba Urusi inajiandaa kuongeza mashambulizi wiki hii wakati taifa hilo likisubiri uamuzi wa kihistoria wa Umoja wa Ulaya juu ya ombi la kujiunga na umoja huo. Zelensky hata hivyo amesema wanajiandaa na wako tayari na hatua hiyo ya Urusi. Amesema hayo siku moja baada ya ziara ya nadra nje ya mji wa Kyiv ambako alikutana na kuwasalimia wanajeshi kwa mara ya kwanza tangu Urusi ilipolivamia taifa hilo. Amesema katika video aliyoirusha kwenye mtandao wa Telegram wakati akirejea Kyiv ya kwamba kamwe hawatamuachia yoyote eneo la kusini na kuahidi kurejesha kila kilichochukuliwa. Katibu mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Jens Stoltenberg tayari ameonya kwamba vita hivyo vitadumu kwa muda mrefu na kuyaomba mataifa ya magharibi kujiandaa kutoa misaada ya muda mrefu ya kijeshi, kisiasa na ya kiuchumi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu