Haye ataka kukipiga kwa mara nyingine na Bellew.

In Kimataifa, Michezo

 

Bondia David Haye amesema yupo tiyari kurudia mpambano na Tony Bellew.

Mpambano wao wa raundi 11 uliishia raundi ya 6 walipokutana mwezi Machi.

Haye alipigwa ndani ya raundi ya sita kwa makonde ya mfululizo yaliyompeleka chini.

Ameandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba” imechukua miezi kadhaa ya majadiliano na sasa ni muda wa kwenda tena ulingoni”

Hakuna tarehe wala sehemu kamili mpambano huo utakapofanyika, lakini baadhi ya taarifa zinasema utafanyika Disemba 17, kwenye uwanja wa London O2.

Haye alifanyiwa upasuaji baada ya kuchapwa vibaya na Bellew mzaliwa wa Liverpool na tokea kupona kwake amekuwa akifanya mazoezi na walimu wake Shane McGuigan.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu