Mamlaka ya Mapato TRA yakusanya shilingi trilioni 10.87 ndani ya miezi 9

In Kitaifa

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa ripoti ya mapato yaliyokusanywa ndani ya miezi 9 kuanzia June 2016 hadi March 2017 ambayo ni Shilingi Trilioni 10.87 ikiwa ni ongezeko la asilimia 9.99 ukilinganisha na mwaka uliopita.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo

Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo alisema zaidi ya Shilingi Trilioni 1.34 zilikusanywa katika mwezi March 2017 pekee ikionesha kupanda kwa asilimia 2.23 ukilinganisha makusanyo ya mwezi kama huo mwaka 2016 ambapo zilikusanywa Shilingi Trilioni” 1.31.

“Katika kipindi cha miezi 9 ambayo imeanzia mwezi wa June 2016 hadi mwezi Marchi 2017, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi Trilioni 10.87 za Kitanzania hayo ni makusanyo ya miezi tisa,”alisema Kayombo.

Aliendelea kufafanua kuwa, “Katika mwezi wa Machi 2017 TRA imekusanya jumla ya shilingi trilioni 1.34 ukilinganisha trilioni 1.31 ya mwezi machi 2016 ambayo ni sawa na aslimia 2.23. Pamoja na mafanikio tuliyoyapata katika kipindi cha miezi tisa iliyopita, katika kipindi cha miezi mitatu kilichobaki TRA itahakikisha inakusanya kodi mbalimbali ili kufikia lengo la kukusanya trilioni 15.1 kwa mwaka.”

Aidha Katika hatua nyingine, Kayombo amesema TRA inaendelea na mpango wake wa kukusanya kodi za majengo kwa kutoa viwango maalumu vya kodi kwa majengo ambayo bado hayajafanyiwa tathimini.

NINI MAONI YAKO???? COMMENT HAPA CHINI

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu