Boko haram wajilipua, watu 16 wauawa.

In Kimataifa
Watu 16 wameuawa Kaskazini Mashariki mwa nchi ya Nigeria baada ya magaidi wa kundi la Boko Haram kujilipua katika mji wa Maiduguri katika jimbo la Borno.
Shambulizi hili limethibitishwa kutokea na Shirika la taifa la kushughulikia mizozo NEMA.
Msemaji wa Shirika hilo Abdulkadir Ibrahim amesema waliotekeleza shambulizi hilo lilitekelezwa na wanawake wawili waliokuwa wamejifunga mabomu mwilini.
Aidha, amesema kuwa miongoni mwa watu hao 16 waliopoteza maisha, ni washambuliaji hao.
Kundi la Boko Haram limeendelea kuwa tishio kwa raia wa Kaskazini mwa nchi hiyo na mataifa jirani.
Mamia ya watu wamepoteza maisha Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo tangu kuanza kwa mwaka huu.
Shambulizi la hivi karibuni lilitokea mapema mwezi huu na kusababisha vifo vya watu 11 karibu na mji wa Maiduguri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu