Boko haram wajilipua, watu 16 wauawa.

In Kimataifa
Watu 16 wameuawa Kaskazini Mashariki mwa nchi ya Nigeria baada ya magaidi wa kundi la Boko Haram kujilipua katika mji wa Maiduguri katika jimbo la Borno.
Shambulizi hili limethibitishwa kutokea na Shirika la taifa la kushughulikia mizozo NEMA.
Msemaji wa Shirika hilo Abdulkadir Ibrahim amesema waliotekeleza shambulizi hilo lilitekelezwa na wanawake wawili waliokuwa wamejifunga mabomu mwilini.
Aidha, amesema kuwa miongoni mwa watu hao 16 waliopoteza maisha, ni washambuliaji hao.
Kundi la Boko Haram limeendelea kuwa tishio kwa raia wa Kaskazini mwa nchi hiyo na mataifa jirani.
Mamia ya watu wamepoteza maisha Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo tangu kuanza kwa mwaka huu.
Shambulizi la hivi karibuni lilitokea mapema mwezi huu na kusababisha vifo vya watu 11 karibu na mji wa Maiduguri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu