Jeshi la polisi lafyeka ekari 2 za shamba la bangi.

In Kitaifa
Jeshi la polisi wilaya na mkoa wa Lindi limefanikiwa kufyeka na kuteketeza shamba la bangi lenye ukubwa wa zaidi ya ekari mbili,na kukamata lita 177 za pombe haramu aina ya gongo na kuwashikilia jumla ya wanaume kumi na wanawake saba.
Ikiwa ni operesheni ya kawaida zinazofanywa na jeshi la polisi wilaya ya Lindi na ushirikiano wa raia wema, kikosi maalum kilifanya msako katika kijiji cha Mnali na kufanikiwa kukuta shamba lililosheheni miche ya bangi.
Jeshi la polisi likiongozwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi mwandamizi,Renatha Mzinga pamoja na kufuata taratibu za kisheria , waliteketeza shamba hilo.
Kwa mujibu wa sheria , Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Lindi Erasto Yakobo Phili alishuhudia uwepo wa shamba hilo na kuamuru kuteketezwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu