Jeshi la polisi lafyeka ekari 2 za shamba la bangi.

In Kitaifa
Jeshi la polisi wilaya na mkoa wa Lindi limefanikiwa kufyeka na kuteketeza shamba la bangi lenye ukubwa wa zaidi ya ekari mbili,na kukamata lita 177 za pombe haramu aina ya gongo na kuwashikilia jumla ya wanaume kumi na wanawake saba.
Ikiwa ni operesheni ya kawaida zinazofanywa na jeshi la polisi wilaya ya Lindi na ushirikiano wa raia wema, kikosi maalum kilifanya msako katika kijiji cha Mnali na kufanikiwa kukuta shamba lililosheheni miche ya bangi.
Jeshi la polisi likiongozwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi mwandamizi,Renatha Mzinga pamoja na kufuata taratibu za kisheria , waliteketeza shamba hilo.
Kwa mujibu wa sheria , Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Lindi Erasto Yakobo Phili alishuhudia uwepo wa shamba hilo na kuamuru kuteketezwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu