Jeshi la polisi lafyeka ekari 2 za shamba la bangi.

In Kitaifa
Jeshi la polisi wilaya na mkoa wa Lindi limefanikiwa kufyeka na kuteketeza shamba la bangi lenye ukubwa wa zaidi ya ekari mbili,na kukamata lita 177 za pombe haramu aina ya gongo na kuwashikilia jumla ya wanaume kumi na wanawake saba.
Ikiwa ni operesheni ya kawaida zinazofanywa na jeshi la polisi wilaya ya Lindi na ushirikiano wa raia wema, kikosi maalum kilifanya msako katika kijiji cha Mnali na kufanikiwa kukuta shamba lililosheheni miche ya bangi.
Jeshi la polisi likiongozwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi mwandamizi,Renatha Mzinga pamoja na kufuata taratibu za kisheria , waliteketeza shamba hilo.
Kwa mujibu wa sheria , Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Lindi Erasto Yakobo Phili alishuhudia uwepo wa shamba hilo na kuamuru kuteketezwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu