FIFA na UEFA Wapanga Mkakati kumaliza Figisu za Soka Ulaya

In Michezo
Vuta nkuvute kati ya Shirikisho la Mpira Duniani FIFA na Shirikisho la soka Barani Ulaya UEFA bado ni mbichi kwani Rais wa UEFA Aleksander Ceferin amezishutumu ligi kubwa za Ulaya kwa kujaribu kushirikiana kulilaghai shirikisho hilo kwenye mambo mbalimbali hasa ushiriki wa vilabu vyao kwenye mashindano ya Ulaya .

Chama  hicho kinachowakilisha ligi za Ulaya ambacho kina wanachama kutoka katika nchi 25 maarufu kama (EPFL), kimekua kikienda kinyume na kuipinga UEFA tangu kuachwa kushirikishwa kwenye mabadiliko ya maingizo kwenye klabu bingwa Ulaya na mgawanyo wa fedha za washindi.

Awali kulikuwa na makubaliano kati ya EPFL na UEFA juu ya kuepuka ligi kuingiliana yalimalizika muda wake mwezi uliopita, na EPFL wakasema ligi zake kwa sasa zitakuwa huru kuweka mechi katika muda unaofanana na ule wa klabu bingwa Ulaya na mechi za Europa League.

Image result for helsinki finland Aleksander Ceferin and Infantino

                        Rais wa UEFA Aleksander Ceferin

Haiwezekani kufikiria na kuingia mtego wa ulaghai kutoka kwa wale wanaoamini kuwa wanaweza kuzizunguka na kuzitumia ligi ndogo katika kutaka kuweka adhima yao ndani ya mashirikisho kadhaa kwa sababu tu wanaamini wanaweza kufanya hivyo kutokana na nguvu wanayopata kutokana na mapato ambayo ligi za ndani za nchi zao zinaingiza, Ceferin alisema kwenye mkutano wa UEFA mapema leo  jijini Helsinki nchini Finland.

 

 

Rais wa FIFA  Gianni Infantino alihudhuria mkutano huo na kusema kuwa  uchaguzi uliomweka Ceferin madarakani mwaka jana ulimaliza uadui uliokuwepo katia ya UEFA na FIFA,Kwa kusema “Huu ni upinzani wa kipuuzi kati ya UEFA na FIFA ambao haupo tena na ambao hautakiwi kuwepo,

Kwa muongo mmoja sasa shirikisho la Soka Duniani limekuwa likilaumu shirikisho la Soka barani Ulaya UEFA kuwa linapoteza fedha nyingi kwa njia isiyojulikana hususani kwenye mapato kitu ambacho FIFA imekiita kama ufujaji wa pesa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu