FIFA na UEFA Wapanga Mkakati kumaliza Figisu za Soka Ulaya

In Michezo
Vuta nkuvute kati ya Shirikisho la Mpira Duniani FIFA na Shirikisho la soka Barani Ulaya UEFA bado ni mbichi kwani Rais wa UEFA Aleksander Ceferin amezishutumu ligi kubwa za Ulaya kwa kujaribu kushirikiana kulilaghai shirikisho hilo kwenye mambo mbalimbali hasa ushiriki wa vilabu vyao kwenye mashindano ya Ulaya .

Chama  hicho kinachowakilisha ligi za Ulaya ambacho kina wanachama kutoka katika nchi 25 maarufu kama (EPFL), kimekua kikienda kinyume na kuipinga UEFA tangu kuachwa kushirikishwa kwenye mabadiliko ya maingizo kwenye klabu bingwa Ulaya na mgawanyo wa fedha za washindi.

Awali kulikuwa na makubaliano kati ya EPFL na UEFA juu ya kuepuka ligi kuingiliana yalimalizika muda wake mwezi uliopita, na EPFL wakasema ligi zake kwa sasa zitakuwa huru kuweka mechi katika muda unaofanana na ule wa klabu bingwa Ulaya na mechi za Europa League.

Image result for helsinki finland Aleksander Ceferin and Infantino

                        Rais wa UEFA Aleksander Ceferin

Haiwezekani kufikiria na kuingia mtego wa ulaghai kutoka kwa wale wanaoamini kuwa wanaweza kuzizunguka na kuzitumia ligi ndogo katika kutaka kuweka adhima yao ndani ya mashirikisho kadhaa kwa sababu tu wanaamini wanaweza kufanya hivyo kutokana na nguvu wanayopata kutokana na mapato ambayo ligi za ndani za nchi zao zinaingiza, Ceferin alisema kwenye mkutano wa UEFA mapema leo  jijini Helsinki nchini Finland.

 

 

Rais wa FIFA  Gianni Infantino alihudhuria mkutano huo na kusema kuwa  uchaguzi uliomweka Ceferin madarakani mwaka jana ulimaliza uadui uliokuwepo katia ya UEFA na FIFA,Kwa kusema “Huu ni upinzani wa kipuuzi kati ya UEFA na FIFA ambao haupo tena na ambao hautakiwi kuwepo,

Kwa muongo mmoja sasa shirikisho la Soka Duniani limekuwa likilaumu shirikisho la Soka barani Ulaya UEFA kuwa linapoteza fedha nyingi kwa njia isiyojulikana hususani kwenye mapato kitu ambacho FIFA imekiita kama ufujaji wa pesa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu