Hoteli ya kifahari ambayo ni gereza kwa wanawafalme Saudi Arabia.

In Kimataifa

Ni jina la mahoteli ya kifahari yaliyo maarufu kote duniani.

Marais, mawaziri wakuu na wafalme wamekaribishwa katika mahoteli ya Ritz-Carlton.

Lakini kwa mujibu wa ripoti kadhaa, mahoteli hayo katika mji mkuu wa Saudi Arabia yamekuwa gereza.

Miezi michache baada ya kumkaribisha Rais wa Marekani Donald Trump wakati wa ziara yake ya kwanza kama rais, watu kadhaa mashuhuri nchini Saudi Arabia sasa wanaripotiwa kuwa wageni wa serikali huku hoteli hiyo ikitajwa kuwa gereza la kifahari zaidi duniani.

Wanawafalme 11, mawaziri wanne na watu wengine kadhaa wamekamatwa katika kile mamlaka za saudi Arabia zinasema kuwa ni kampeni ya kupambana na ufisadi nchini humo.

Bilionea maarufu duniani Prince Alwaleed bin Talal anaripotiwa kuwa miongoni mwa wale waliokamatwa.

Mtandao wa gazeti la The New York Times ulichapisha kanda ya video iliyoonyesha wajibu mpya wa hoteli ya Ritz-Carlton Riyadh.

Katika video hizo walinzi wanaonekana wamelala kwenye mikeka katika chumba kimoja cha hoteli, watu wenye sare pia nao wanaonekana huku bunduki zikionekana zikiegeshwa kwenye ukuta.

Gazeti la Guardian liliripoti kuwa wageni waliombwa siku ya Jumatano jioni wakusanyike sehemu moja na mizigo yao, kabla ya kusafirishwa kwenda kwa hoteli zingine mjini Riyadh.

The Guardian inamnukuu afisa mmoja wa Saudi Arabia akisema kuwa mamlaka hazingeweza kuwaweka watu hao gerezani na hilo lilikuwa suluhu bora.

Jitihada za kulipia vyumba katika hoteli hiyo siku ya Jumannwe hazikuzaa matunda.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu